Monday, May 13, 2013

FIDIA KWA MADHARA YATOKANAYO NA UZEMBE WA MTU MWINGINE

SWALI: Je, naweza klushtaki iwapo A anafanya uzembe inaosababisha madhara kwangu au mali yangu?

NDIYO: Kama mna mkataba unaweza kushtaki kwa kutumia vipengele vya ukiukwaji mkataba. Unaweza pia kuleta mashtaka sambamba na hili, ama pia kama huna mahusiano ya maktaba na huyo aliyekutenda, kwa kutumia Sheria za Madhara ziitwazo 'Torts'. Misingi ya makosa ya uzembe imefafanuliwa katika hukumu maarufu ya Donoghue v. Stevenson na nyinginzeo kama Blythe v. Birmigham Water Works ambapo Jaji Bwanyenye Aderson (Lord Alderson) alifafanua nini maana ya uzembe kisheria:

"Kutokufanya jambo ambalo mtu mwenye akili ya kawaida angepaswa kulifanya ama kufanya jambo ambalo mtu mwenye akili ya kawaida angeepuka asilifanye"

Na pia angalia hukumu ya Lord Esher katika Le Lievre Dhidi ya Gould [1891] 1 Q.B. 491 iliyohukumiwa na Kitengo cha Utoaji haki cha Malkia wa Uingereza (Q.B.D)

No comments:

Post a Comment