Monday, May 13, 2013

SHERIA ZA JINAI TANZANIA


WEWE: Sheria zipi zinatawala masuala ya jinai Tanzania?

DENIS MARINGO:  Zipo Sheria kadhaa lakini Sheria ziliyo Kuu na muhimu zaidi kwa masuala ya jinai na Tanzania nya Kwanza ni Ile iitwayo Penal Code (cap. 16) kama ilivyozoeleka kimombo. Kwa Kiswahili Sheria hii huitwa KANUNI YA ADHABU na hata kama utasema tu SURA YA 16 Ya Sheria za Tanzania mwanasheria yeyote atakuelewa na hata mahakama inayosikiliza kesi yako ya jinai ama nduguyo itakuelewa pia.   Sheria hii inaumba makosa takribani yote unayoyajua ni jinai (wizi, mauaji, ubakaji, uhaini na kadhalika) na pia inatamka adhabu kwa takribani kila kosa inaloliumba humo.

kama nilivyodokeza zipo sheria nyinginezo pia.Mathalani, SHERIA YA MWENENDO WA MAKOSA  JINAI, kimombo ikifahamika kama CRIMINAL PROCEDURE ACT, ni muhimu sana ewe Mtanzania ukainunua na ukaisoma na kuilewa. Kwa nini?  taratibu za wewe ama nduguyo kukamatwa ama kuhojiwa na polisi ama mamlaka za dola zimo humo. Utoaji dhamana kwa watuhumiwa umefafanuliwa humo. Polisi anapaswa afuate yale yaliyoelekezwa humo pale anapotaka kukusaili ama kukufanyia upekuzi nyumbani ama katika gari lako na mahali popote nchini. yamo mengi zaidi ya hayo katika sheria hii ambayo falsafa yake ilikuwa ni kumlinda raia na haki zake pale anapokabiliwa na tuhuma za jinai na pia kudhibiti matumizi yasiyofaa ya utumiaji nguvu za dola.

Na tena nimefafanua kuwa zipo sheria zaidi kama ile ya Minimum Sentemcing Act, 1972 ambayo inaweka misingi ya Utoaji adahabu kwa wale waliotiwa hatiani. je uende gerezani/ chuo cha mafunzo na kwa muda gani. yamo humo. Utandikwe mijeledi ama la? Hilo ni kosa lako la kwanza, je utastahili kutumikia adhabu sawa na mtu aliyetenda kama wewe lakini kakubuhu katika jinai? Yamefafanuliwa humo.

Na pia tena takribani kila sheria nyinginezo huwa zinatoa adhabu katika kifungu kimoja, viwili au vitatu hivi. heria ya Uchaguzi ya mwaka 1985 imebeba jinai katika amsuala ya kutaka kuvuruga uchaguzi na kadhalika. Sheria za Filamu zina vifungu vya jinai kuhusu uonyesha picha za ngono. Sheria za barabarani zina jinai kuhusu uendeshaji magari hatarishi ama kuendesha bila bima ya lazima. Sheria za utangazaji zaweza na hakika zina jinai kuhusu uchochezi. Sheria za kuabudu vile vile vile Sheria za Elimu zina jinai kuhusu wizi wa mitihani. Sheria za Benki zina jinai kuhusu masuala ya utakatishaji fedha na kadhalika. Hii ni mifano tu.

No comments:

Post a Comment