Monday, May 13, 2013

ZUIO LA MAHAKAMA (INJUNCTION) NI KITU GANI? (LUCAS MATAFU v. MUSTAFA SONGAMBELE)[1977] LRT 10

WEWE: Nini maana ya Injunction. Tusaidiane katika lugha yetu ya Taifa.

DENIS MARINGO: Una maana gani uaposema lugha ya Taifa. Nasema hivi kwa vile KIINGEREZA ni Lugha ya Taifa pia kwa mujibu wa Katiba yetu. Ningekujibu kwa Kiswahili ama Kiingereza kwa vile zote ni lugha za Taifa-Kwa mujibu wa Katiba! Nimekusoma pengine unahitaji maelezo Kiswahili.

Injunction ni amri ya mahakama ambao 'inazuia' jambo fulani lisifanyike na yule 'anayetaka kulifanya'.
honde chonde, zingatia sana hicho nilichoki-bold na kukupigia mstari kwa maana msisitizo. Wapo Wana sheria wenye kufikiri kimakosa kuwa injunction ni amri ya mahakama. Hii haitoshi. Haitoshi kwa sababu amri yaweza kuamru jambo lifanyike ama lisifanyike. Injunction haifiki huko. Injunction ni kitu cha Magharibi tu, hakiendi Mashariki. Ni kitu cha Kushoto-kamwe hakielekei kuumeni. Nina maana gani?

Kusema kweli nashukuru sana hekima za hayati Jaji Lameck MFALILA kwa uamuzi ulijaa busara kubwa katika shauri alilohukumu la Lucas Matafu v. Hon. M. M. Songambele[1977] LRT 10


Hata siku moja, na kamwe, Injunction haijawahi kumaanisha amri ya kufanyika jambo. injunction hukata tu kwa kuzuia. Ki-msingi injunction inakuwa na maana tu pale inapokidhi mambo haya mawili (la tatu na muhimu zaidi na ambalo lingepaswa kuwa la kwanza, silitaji hapa kwa sasa):

(1) Injunction itatolewa na mahakama kama kile kinachotakwa kizuilike kufanyike bado hakijafanyika. Maana yake ni kuwa utakuwa mwendawazimu kuomba injunction kumzuia mtu asitangaze matokeo ya uchaguzi kama tayari kura zimechakachuliwa na matoke yamrtangazwa ama kuzuia nyumba isiuzwe ama kubomolewa wakati haya yameshafanyika!

(2) Ewe Wakili iombe Mahakama itoe Injunction 'KUZUIA JAMBO LISIFANYIKE' na si 'KUSHINIKIZA JAMBO LIFANYIKE'.  Injunction ni kuzuia na si kuamrisha!

No comments:

Post a Comment