Monday, May 20, 2013

HAKI YA KUKATA RUFAA TANZANIA

SWALI: Rufaa ni nini? Sheria gani inahusika na masuala ya Rufaa Tanzania?

DENIS MARINGO: Rufaa ni wasilisho mahakamani ambapo upande fulani usioridhika na hukumu iliyotolewa huiomba mahakama ya juu kupitia upya na kurekebisha ama kutengua hukumu husika.
Zipo heria kadhaa zinazotoa haki ya kukata rufaa. Sheria hizi zaweza kua zile zinazohusu kesi zote kwa ujumla nchini, kama ilivyo heria ya Mahakama za Mahakimu ya mwaka 1984. chini ya sheria hii maamuzi ya mahakama za Mwanzo hukatiwa rufaa mahakama za Wilaya ama hakimu Mkazi.Maamuzi haya nayo yaweza kukatia Rufaa Mahakama Kuu.

Uamuzi wa Mahakama Kuu unaweza kukatiwa Rufaa Mahakama ya Rufaa ambapo ndipo ukomo ulipo. Mifano ya maamuzi muhimu yaliyofika Mahakama ya Rufaa na kutoa ufafanuzi wa kina wa heria husika ni pamoja na Bi. Hawa Mohamed v. Ally Sefu [1983] TLR 32 ambayo ilihusika na mgawanyo wa mali ndoa inapovunjia pamoja na shauri la Kukutia Ole Pumbun [1994] lililohusika na mashtaka yanayoletwa dhidi ya Serikali. Angalia pia hukumu katika rufaa za Daudi Pete; Lohay Akooonay, Agnes Doris Liundi na nyinginezo muhimu.

Muhimu kukumbuka kuwa haki ya Kukata rufaa ni ya Kikatiba kuitia ibara 13(6)(a) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.



No comments:

Post a Comment