Monday, May 13, 2013

HUKUMU YA AGNES DORIS LIUNDI INA UMUHIMU GANI TANZANIA?

WEWE: Nimesikia sikia kutajwa kwa hukumu ya Agnes Doris Liundi. Inahusika na nini?

DENIS MARINGO: Zipoi Hukumu mbili za Agnes Doris Liundi na zote mbili zina umuhimu mkubwa katika masuala ya Sheria za Jinai Tanzania. Unazungumzia ipi kati ya hizo. Basi niweke tu mambo sawa kwa kusema kuwa zote mbili zilihukumiwa na Mahakama za juu Tanzania japo zinatofautiana kwa mamlaka. ya Kwanza ilihukumiwa na Mahakama Kuu na hiyo inaitwa JAMHURI v. AGNES DORIS LIUNDI na ya pili ikawa ni rufaa ya Bibi Agnes mbele ya Mahakama ya Rufaa akiomba hukumu dhidi yake itenguliwe. Hii ya Pili iko sahihi kama utaitaja AGNES DORIS LIUNDI v. JAMHURI. Kumbuka, kisheria yule anayewasilisha malalamika kama mshtaki wa awali ama mkataji rufaa jina lalke hutajwa mwanzao na yule anayeshtakiwa ama kukatiwa rufaa dhidi yake hufuatam na ndiyo mantiki ya tifauti hii hapo Juu. Turejee katika swali lako.

Bibi Agnes Doris Liundi alikuwa mke wa Balozi Liundi na mwishoni mwaka 1979 aliwaua wanawe wadogo watatu-kati ya wanne- kwa kuwatumbukiza majini nyumbani kwake Keko, Temeke,  Dar es Salaam baada ya kuonekana kuwa amechanganyikiwa kwa atahri za mgogoro wa unyumba na mumewe. Jamhuri ikamshtaki kwa makosa ya kuua kwa kukusudia na hii ndiyo kesi iliyokuwa Mahakama Kuu ya Tanzania na ikatolewa hukumu na Jaji Lewis Makame amabye hakukubaliani na utetezi wa Bibi Liundi kuwa alikuwa akiugua wazimu (Insanity) alipotenda kosa hilo. msingi wa utetezi huu ni hukumu maarufu ya Uingereza iitwayo M'naughten ambayo inatumika kote ulimwenguni.

Ndipo alipokata rufaa mahakama ya Rufaa ambapo mahakama hiyo pia ikakataa utetezi wake. Kwa hivyo basi hukumu hii ni muhimu kuelewa dhana kadhaa kama vile a kuua kwa kukusudia, kuua bila kukusudia, utetezi wa wazimu (insanity plea) na nafasi ya ushahidi wa kitabibu (Medical evidence) katika kesi za jinai.

No comments:

Post a Comment