Monday, May 13, 2013

NAFUU YA FIDIA KWA KUBAMBIKIZIWA KESI NA KUSHTAKIWA MAKUSUDI

SWALI: Je, naweza kumshtaki raia mwenzangu, polisi ama ofisa anayenibambikizia kesi kwa lengo la kunikomoa na hatimaye nikashtakiwa jinai kwa makusudi na hila japo sikuwa na hatia yoyote?

DENIS MARINGO: Ndiyo waweza. Jambo hili limefafanuliwa mahali pengi na pia katika hukumu ya Festo Dhidi ya Mwakabana (1971) HCD n.417 na ile ya Hosia Lalata Dhidi ya Gibson Zumba Mwasote [1980] TLR 154. Kesi za kubambikiziana ama kukomoana chimbuko lake ni hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Kibwanyenye ya Uingereza (House of Lords) katika shauri maarufu la Herniman v. Smith [1938] A.C. 305

No comments:

Post a Comment