Monday, May 13, 2013

MWAJIRI AWEZA KUWAJIBIKA KWA MAKOSA YA MWAJIRIWA?

WEWE: Bwana Sheria. Je inawezekana kweli kumshtaki mwajiri kwa jambo linalota madhara kwa mwingine ambapo mwajiri mwenyewe hajafanya kosa ila limefanywa na mwajiriwa? Mathalani, Je naweza kuumia kwenye basi nikamshtraki mmiliki kwa kutokuwa makini katika kuajiri dereva mzembe na asiye na taaluma, kiwango au mafunzo?

DENIS MARINGO: Swadakta. Hilo lawezekana japo si mara zote kwa vile lina misingi na mipaka yake. Kisheria nadharia hii inajulikana kama 'Vicarious liability' (liability of the Master by the Acts/Omissions) of his Servant. Wamombo wanaamanisha hapa kuwa 'Uwajibikaji kisheria wa Mwajiri/Bwana katika makosa ya Mwajiriwa/Mfanayakazi. Enzi za Ukabaila ama Utumwa tungeweza kuongezea 'Mtwana' pia. Kwa Tanzania nadharia hii ilifafanuliwa vema na Mahakama Kuu katika hukumu ya Anglina v. Nsubuga na Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba (1971) HCD n. 190

No comments:

Post a Comment