Monday, May 13, 2013

HUKUMU YA DAUDI PETE [1993] TLR NA MISINGI YA DHAMANA KMA HAKI YA KIKATIBA

WEWE: Hii hukumu ya Daudi Pete nimeisikia hapa na pale. Nini kitu hiki?

DENIS MARINGO: Hukumu hii ya Daudi Pete [1993] TLR ilitolewa mwanzoani mwa miaka ya tisini na na mahakama zetu za juu inahusika na utolewaji wa Dhamana kama haki ya Kikatiba. Ilifafanuliwa kupitia hukumu hii kuwa Dhamana ni haki ya Kikatiba na isinyimwe pasipo sababu nzito na za msingi kwa sababu Katiba inatamka kuwa mtuhumiwa wa kosa anapaswa kuhesabika hana hatia hadi anapothibitishwa na mahakama yenye mamlaka husika kuwa ametenda kosa hilo, ispokuwa pia kwa makosa mazito na makubwa ambayo utolewaji wake umewekewa kigingi na Sheria husika. makosa haya ni kama kuua kwa kukususia (murder) na uhaini (treason).

No comments:

Post a Comment