Monday, May 13, 2013

SHERIA KUHUSIANA NA NDOA TANZANIA NI ZIPI?


WEWE: Sheria zipi zinatawala masuala ya ndoa Tanzania?

DENIS MARINGO:  Zipo Sheria kadhaa lakini Sheria iliyo Kuu na muhimu zaidi kwa masuala ya ndoa na familia inaitwa Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971. Inarejewa pia kama Sheria namba 5 ya mwaka 1971 na ni maarifu zaidi miongoni mwa wanasheria ndani na nje ya mahakama kwa jina la Law of Marriage Act, 1971. Sheria hii moja kwa moja inatawala ndoa za Kiseerikali na zile za kidini na pia zile za kimila kama zilivyoanishwa katika matangazao mawili muhimu ya Serikali ya mwaka 1963 kuhusiana na ndoa, talaka na ugawanaji mali na wato kimila. Kwa Ndoa za Kiislam, Sheria za Kiislam zinafuatwa na kuhesjimiwa na mahakama kama wanandoa husika wamefunga ndoa kwa kufuata imani ya dini hii. 

No comments:

Post a Comment