Monday, May 13, 2013

TARATIBU ZA KUISHTAKI SERIKALI YA TANZANIA MAHAKAMANI

SWALI: Je, mimi kama Mtanzania naweza kuishtaki Serikali yangu hii ya Tanzania kama naona imenitenda jambo baya ama imekiuka yenyewe Sheria zetu na Katiba ya nchi yetu?

DENIS MARINGO: Ndiyo, waweza. Hata hivyo umeshatamka mwenyewe 'Serikali'. Kuishtaki dola si jambo jepesi lakini mara kwa mara linafanyika na hata serikali kuonekana imevunja sheria zake yenyewe ama  Katiba.Taratibu za kuishtaki Serikali zimefafanuliwa katika Katiba na Sheria nyinginezo kama Governnment Proceedings Act. Na pia kuna Sheria kama The Basic Rights and Duties Enforcement Act, 1994 ama nyinginezo kama Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Madai (Civil Procedure Code Act). Watafute wanasheria wakusaidie kwa ufafanuzi.  Muhimu hata hivyo ni kuwa ujue unachoshtakia kama kitakubalika na mahakama, ujue ni mahakama ipi utapeleka jambo lenyewe na pia utoe taarifa (notis) ya awali kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kulingana na misingi iliyoanishwa katika hukumu za  Peter Ngh'omango dhidi ya Gerson Mwangwa [ 1993] TLR  na ile ya Kukutia Ole Pumbun na Mwenzake Dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Tanzanial; ile ya mfanyabiadhara Lucas Matafu Dhidi ya Mheshimiwa Mustafa Songambele [1976] LRT n.10 ; na nyinginezo kadhaa. Zamani ulipaswa kuomba idhini Serikali yenyewe kuwa unakusudia kuishtaki lakini jambo hili lilibatiliwa na Mahakama kwa kuonekana kukiuka Katibam na hasa ibara ya 13(6)(a) .

No comments:

Post a Comment