Monday, May 13, 2013

KUHUSU BLOGU HII

Kuelimisha Umma wa Tanzania kuhusiana na Sheria za nchi hii na hukumu muhimu zilizotafsiri sheria hii.

Kuwasilisha hukumu hizi kwa lugha ya KISWAHILI kwa kutumia tafsiri zangu mwenyewe na pia tafsiri yako wewe Msomaji na wapenzi wengine watakaofuatilia hapa.

Kuwasilisha makala/maandiko niliyowahi kuandika katika Vyuo vikuu nilikosomea Taaluma hii na marejeo niliyoawahi kujisomea nikiwa katika nchi hizi tatu (Mlimani-anzania,  Marekani na Uholanzi)

Kukosoa, kwa ushirikiano na watanzania wenzangu, mapungufu yaliyomo katika Sheria zetu ili kujenga taifa lnye utawala bora wa sheria, kuondoa urasimu na ukiritimba wa kisiasa, kiutawala na kuimarisha demokrasia, haki na fursa kayika nyanja zote kwa Watanzania wote bila kujali umri, jinsi, dini, kabila, nasaba, rangi ya mtu, elimu, mahali anapoishi, hali ya kiuchumi, shughuli aifanyayo na kadhalika.

Kuwatambua watanzania waliotoa mchango muhimu katika kuimarisha dhana ya uytawala bora na utawala wa sheria na poia utetezi wa haki za binadamu nchini.

Kufanya mambo mengine yoyote ambayo yatachochea malengo haya hapo juu kwa kuzingatia kutovunja Sheria zisizokinxana na misingi ya katiba na haki za binadamu.

TUANZE KAZI!!!

No comments:

Post a Comment