Monday, May 13, 2013

SHERIA ZA ARDHI TANZANIA

WEWE: Sheria zipi zinahusiaka na Ardhi Tanzania.

DENIS MARINGO:Inategemea unazungumzia ardhi ipi na iko wapi ama jambo gani kuhusiana na ardhi husika. Kifupi naweza tu kukuridhisha kuwa Ardhi si suala la Muungano. tanzania bara wana Sheria za ardhi na Zanzibar pia wanazo zao kwa masuala ya huko. Kimsingi, hata hivyo, kwa Tanzania bara, sheria maarufu ya ardhi ya mwaka 1923 (Land Ordinance) haipo tena. tangu mwaka 1999 Bunge lilitunga Sheria mbili muhimu katika jambo hili. Sheriaya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 inatawala masuala muhimu na ya ujumla ya ardhi Tanzania. Sheria namba 5 ya mwaka 1999 inahusika zaidi katika ardhi iliyo katika himaya ya Kimila ama Vijiji. Sheria Nyingine muhimu ni Sheria ya Uandikishaji Ardhi. Je ni hizi tu? usipotoke. Umetokea mgogoro wa ardhi unakimbilia wapi na utatuzi unakuwaje? Ipo sheria katika hili-nayo yaitwa Sheria ya Mahakama za Adhi ya mwaka 2002.

Kwa vile pengine wewe si Mwanasheria usijiridhishe kwamba umeshajua sasa sheria hizi kwa kusoma hicho nilichodonia hapo juu. Wamombo wangesema 'that's just a tip of an iceberg!.  Basi nakusihi ndugu yangu tafuta mwanasheria makini katika ufafanuzi wa masuala haya ili usije ukabaini imepoteza haki yako kwa kutowatafuta wale waliofundishwa kukusaidia wewe. Je, ukiugua Malaria, T.B au gonjwa lolote waweza kujipima na kujitibu? Kama hasha, basi naamini umenielewa. Twende mada nyingine!

No comments:

Post a Comment